WAZIRI MWAKYEMBE ASIKITISHWA NA VIONGOZI WA TFF KUKIMBIA KIKAO

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amesikitishwa na viongozi wa shirikisho la soka Tanzania (TFF) Kuwa na viburi baada ya kuingia mitini na kutohudhuria kikao alichowaita leo hii kujadiliana kilichotokea Afcon na kufukuzwa kwa kocha wa Taifa Stars Emmanuel Amunike.

Dkt.Mwakyembe amesema kama wamemfukuza kocha Emmanuel Amunike kwa kuiga Misri basi waige vizuri, huku akisema Serikali haipingi maamuzi hayo bali iliwaita leo ili watoe mpango mkakati wa sababu ya kumuondoa kocha ambaye hajalipwa takriban miezi mitatu na tunaelekea wapi.

Comments

Popular Posts