Zamaleck watimua kocha kisa kusuluhu mechi

Klabu ya Zamalek ya Misri imemfuta kazi kocha mkuu wa klabu hiyo Christian Gross licha ya kuiwezesha klabu hiyo kutwaa ubingwa wa kombe la Shirikisho barani Afrika .

Rais wa Zamalek Mortada Mansour jana alimpigia simu kocha huyo wa zamani wa Tottenham ya Uingereza na FC Basel ya Uswisi na kumpa ujumbe wa kuondoka haraka nchini humo kufuatia suluhu ya bila kufungana dhidi ya klabu ya  Entag katika mchezo wa ligi kuu ya Misri.

Pichani kocha wa Zamelek  akiwa na  mabegi yake akiondoka nchini Misri

Comments

Popular Posts