STAND YA MABASI YA MIKOANI MBEZI MBIONI KUKAMILIKA

Ujenzi wa stendi mpya ya mabasi yaendayo mikoani na nchi za jirani katika eneo la Mbezi Luis jijini Dar es salaam unaoigharimu Serikali shilingi Bilioni 50.9 umefikia asilimia 57 na umebakiza miezi minne kukabidhiwa.
Ambapo mkandarasi aliyepewa kazi hiyo ya ujenzi wa stendi kutoka Kampuni ya Hainan International ya China ametakiwa kuongeza kasi ili kufikia lengo lililowekwa na serikali.
Stendi hiyo itakakuwa na uwezo wa kuchukua mabasi zaidi ya 700 kwa wakati mmoja, ikiwa ni ongezeko la zaidi ya mabasi 400 ya stendi ya Ubungo.

Comments